Ukisikia Ugogoni lazima utatambua ni katikati ya nchi na makao makuu ya Tanzania, hii ni Dodoma mahali ambapo watarajiwa walichinjiwa na kamwe hawatapasahau. Karibu katika Blog hii ambayo pamoja na mabo mengine inajadili utamaduni halisi wa Mtanzania, karibu!!!
Monday, November 09, 2009
MAMBO YALIKUWA POA




HAWA NI MR & MRS MKISI.COM
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:15 AM | Permalink | Maoni 0

BYEEEEEEEEE


HAOOOOOOOO WANAJIMUVUZISHA!
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:09 AM | Permalink | Maoni 0

Siku Prince Masai alipooa!




WADAU WALIOHUDHURIA SHEREHE YA PRINCE MASAI!
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:03 AM | Permalink | Maoni 0

Siku Prince Masai alipouaga ukapera


Mzee wa SUMO naye alikuwepo jamani!
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:00 AM | Permalink | Maoni 0

Siku Prince Masai alipouaga Ukapera



baadhi ya wadau waliohudhuria harusi ya Prince wakiserebuka!
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 2:57 AM | Permalink | Maoni 0

Siku Mwanablogu ya Prince Maasai ALIPOUAGA UKAPERA

Prince akiwa na Mkewe Elizabeth katika ukumbi wa Kilimani Dodoma.
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 2:23 AM | Permalink | Maoni 0

Monday, September 21, 2009
MAPENZI hayana umri jamani, hebu msome mzee wa miaka 70 aliyejinyonga kwa wivu wa mapenzi!
Na Martha Mtangoo, Dodoma

9/21/2009

MZEE wa miaka 70 aliyefahamika kwa jina la Msuliche Mhogo amejinyonga kwa kutumia kamba kutokana na wivu wa mapenzi.

Kamnda wa polisi mkoani hapa Zelothe Steven aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.30 asubuhi katika kijiji cha Ngh’ambi wilayani Mpwapwa.

Akielezea tukio hilo Kamanda Zelothe alisema kuwa chanzo cha mzee huyo kujinyonga ni kutokana na wivu wa kimapenzi kwa mkewe mwenye umri wa miaka (30) ambaye jina lake limehifadhiwa.

Alifafanua kuwa kwa muda mrefu mzee huyo alikuwa akihisi mkewe ana uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine hapo kijijini ambaye ni jirani yake.

Alisema kuwa awali kabla ya tukio hilo kutokea , usiku mzee huyo aligombana na mkewe kuhusu mtoto wao mmoja ambaye ana umri wa miaka miwili akidai kuwa mtoto huyo ni wa mwanaume ambaye nahisi anatembea naye na si mwanaye.

Kamanda Zelothe alisema kuwa wakati wakiendelea na ugomvi huo mke mkubwa wa mzee huyo alienda kuamua ugomvi huo na ilipofika asubuhi mzee huyo aliaga kuwa anaenda safari na ndipo alipokwenda kwenye mbuyu ambao upo jirani na nyumbani kwake na kujinyonga.

Wakati huohuo jeshi la polisi mkoani hapa linamshikilia Hamis Salum (27) mkazi wa Manispaa ya Moshi kwa tuhuma za kufungua duka na kuiba simu 10 za aina mbalimbali.

Kamanda Zelothe alisema kuwa baada ya kufungua mlango mtuhumiwa huyo alijfungia ndani ya duka hilo na kuanza kukusanya simu dukani humo ambapo mwenye duka ambaye ni Freeman Narcis (23) alifika dukani hapo na alipofungua duka alimkuta mtuhumiwa huyo akiendelea kukusanya vitu katika duka hilo .

Kamanda Zelothe alisema kuwa jeshi hilo bado linamshikilia mtu huyo kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamni mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Ends……
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 4:53 AM | Permalink | Maoni 0

Thursday, August 20, 2009
Ningekuwa Spika Sitta Ningejiuzulu!

NINGEKUWA SPIKA SITTA NINGEJIUZULU

HAKI ya Mungu kweli duniani kuna mambo pamoja na mambo yote mazuri ambayo spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samuel Sitta kwa Wabunge wa chama cha mapinduzi wakiwemo na Mafisadi ambao wanajulikana kwa majina mimi sitaki kuwataja bado wabunge hao ambao wengine ni wajumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (NEC) na mafisadi wamo wamememgeuka!

Jamani kwa kweli ni lazima tukajifunza ustaarabu mengi sita kawasaidia wabunge hawa pamoja na wale wa upinzani lakini sasa tena moto umemgeukia yeye jamani kweli hii ni fair?
Hapa naorodhesha tu mambo machache ambayo spika sitta amewapigania wabunge hawa na kubalansi Bunge ili liliemee upande mmoja halafu akaonekana kana kwamba anapendelea upande mmoja wa CCM!

Spika huyuhuyu ambaye anaitwa Mbabe amepigania kwa nguvu marupurupu ya wabunge na kusababisha sasa hivi wabunge kulipwa mshahara tu kiasi cha sh. Milioni 12 kwa mwezi na marupurupu kibao!

Hiyo haikutosha spika huyohuyo mbabe amepigania mpaka sheria ya kuanzishwa mfuko wa maendeleo ya Jimbo kwa wabunge umepita kwa mbinde Bungeni licha ya wananchi kuonyesha kuukataa!

Mimi sijatumwa na Mtu kuzungumzia hili suala ila nimeguswa na kitendo alichofanyiwa hivi karibuni Mjini Dodoma katika Ukumbi wa Nec wa kutaka avuliwe uanachama kwa kuwa anaendesha eti Bunge kibabe!

Kwa kweli CCM hamkumfanyia Spika wenu sawa kabisa kwa sababu mnataka aliendesheje Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo hivi sasa limekuwa kama Kikundi cha vichekesho cha orijino Komedi kuna jambo lingine zaidi ya hili si mseme?

Alichokisema hivi karibuni Bungeni spika kuwa anaomba ulinzi wa ziada kwa kuwa nguvu ya mafisadi inamzidi alikuwa sahihi kwa kuwa tayati alishaona nini kinafuata na kwa kuwa serikali haikumuelewa ndiyo maana ilipuuzia na maneno meengi ya kejeli yakatolewa juu ya kauli yake!

Lakini ukweli wa maneno ya Mzee Sitta sasa yamejidhihirisha ndani ya mkutano wa CCM ambamo kunaonekana kuwa CCM bila mafisadi haiwezekani kuwa hai, sasa mnataka spika aendesheje Bunge lenu JAMANI?

Mnataka spika atoe uhai wake ndiyo mbaini kuwa alikuwa anaendesha bunge kwa usawa na kubalansi pia au mnatakaje au aendeshe Bunge kwa kupendelea wabunge wa CCM? Mtalishusha hadhi na viwango pia kama mnataka liwe ambavyo ninyi mnataka liwe!
Kwa hali hii mimi ningekuwa Spika Sitta ningejiuzulu Uspika ili kuwaachia nafasi mafisadi kumtafuta spika ambaye wao wanamtaka ambaye hatendesha Bunge kibabe au sio na kupendelea CCM maana viwango ulivyoahidi mwaka ule havitakuwepo tena!

Kwa kweli inauma halafu inakera zaidi inatia kichefuchefu kufanya hivyo ni kuonyesha ni kiasi gani kwamba CCM inashikiliwa na kuendeshwa na watu wachache wenye pesa zao na utartibu huu ambao CCM mmeuonyesha sijui nini kitafuata lakini mmetia DOA tena doa lenyewe jekundu kwenye nguo nyeupe!

SHAURI YENU CCM angalieni msije mkajuta kwa kuwasafisha watu ambao tayari walishachafuka siku nyingi kupitia watu ambao wangekusaidieni kuwasafisha angalau kwa kutumia busara zao ambazo zinaonekana ni ubabe!



 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:15 AM | Permalink | Maoni 0

Tuesday, June 23, 2009
Wasamalia wema wamsaidia Binti Mariam



Picha kushoto; Mwandishi na mmiliki wa Blog hii Martha Mtangoo, akimkabidhi fedha taslim sh. 230,00 Mariam ambaye alikuwa akihitaji msaada kwa ajili ya kufanyiwa operesheni ya saratani ya Jicho ambayo tayari ameshafanyiwa, fedha hizo
ambazo zimetolewa na wasamalia wema Hinai Tamim na Said ambao wanaishi nchini Oman.
Mungu awabariki sana.
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 5:02 AM | Permalink | Maoni 1

Tuesday, May 05, 2009
WENZETU HUKO TARIME wanadumisha mila kwa mtindo huu
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI LAWRANCE MASHA
AMA kweli ukistaajabu ya Mussa uyaona ya Firauni! wakati watu wanapinga mila na desturi zilizopitwa na wakati huko TARIME wenzetu wanadumisha tu!
hebu soma hii kwanza.

Katika mkoa wa Mara kuna mila ambayo imekuwa ikifanywa na wazee wa kimila ambao kutokana na kutekeleza mila hizo matukio ya mauaji yamekuwa yakisababishwa na mapigano ya koo mbalimbali.
Mila hiyo imesababisha hali ya ulinzi na usalama mkoa ni mara kutokuwa shwari na kutoridhisha kutokana na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kuelevya hususan kilimo cha Bangi.
Wazee wa Kimila Mkoani Mara ndiyo viongozi na waamrishaji wa mapigano ya koo yanayondelea, ambapo wazee hao hunufaika na mapigano hayo kwa kupata mgao wa mali zilizoporwa katika mapigano.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrance Masha anasema kuwa mila na desturi za baadhi ya makabila zinachochechea mapigano baina ya vijana wa koo moja na koo nyingine vitendo ambavyo vimekuwa vikiheshimika miongoni mwa jamii hizo kuwa ni vya kishujaa.
Waziri Masha anasema kuwa wazee wa kimila wamekuwa viongozi na waamrishaji wa mapiganmo hayo ambapo wamekuwa na maradaka makubwa katika Koo zao na hutoa adhabu kali kwa vijana wanaokwepa kushiriki mapigano.
Waziri Masha anasema kuwa kutokana na hilo, hadi sasa hali ya ulinzi na usalama katika mkoa wa Mara si ya kuridhisha kwa kuwa kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kulevya hususan kilimo cha bangi.
Anasema kuwa matukio hayo yameenea katika wilaya za Tarime, Rorya na wilaya ya Musoma vijijini ambapo koo za hunyaga na Wamera na koo za Waanchari na Warenchoka na Wakira na Wanyabasi na Wairegi zimekuwa zikipigana mara kwa mara.
Masha anasema kuwa kilimo cha Bangi ambacho kimekuwa ni chanzo kikubwa cha uchumi kwa baadhi ya makabila katika mkoa wa Mara, pia kimekuwa ni chanzo cha mapigano hayo ambapo imekuwa ni kawaida kwa watu katika maeneo hayo kukodishwa na wakala kulima bangi na kulipwa fedha nyingi.
Anasema kuwa pale inapotokea kuwa mkulima wa Bangi aliyekodishwa hakufanikiwa kuvuna Bangi kutokana na Bangi hiyo kuharibika kutokana na ukame au kuharibiwa na vyombo vya dola, mkulima huyo hutakiwa kurudisha fedha alizopewa na wakala wake ambapo ili kupata fedha ya kurudisha, mkulima huiba ng’ombe za koo jirani na kuuza.
Waziri huyo anasema kutokana na mapigano hayo jumla ya watu 136 walifariki na zaidi ya 336 walijeruhiwa huku nyumba 2421 zikichomwa moto na kuacha zaidi ya kaya 756 zikiwa hazina mahali pa kuishi na vihenge 673 vya kuhifadhia mahindi kuchomwa moto katika kipindi cha kuanzia mwaka 2001 hadi machi mwaka huu.
Anazitaja hatua ambazo serikali imeshazichukua kuwa ni pamoja na kuifanya wilaya za Tarime na Rorya kuwa mkoa wa Kipolisi ili kukabiliana ipasavyo na matishio ya usalama, uhalifu na wahalifu.
Hatua nyingine ambayo Waziri Masha anaitaja kuwa ni ile ya serikali ya mkoa kupitia Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), kufanya kampeni mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine zikiwemo za dini, wanasiasa, wizara ya elimu na kushawishi wananchi kuachana na mapigano. Waziri Masha anasema kuwa mikutano ya ujirani mwema baina ya Vyombo vya dola vya Tanzania na Kenya inaendelea kufanyika ili kuimarisha mahusiano miongoni mwao, ambapo mapema mwezi.

HAYA AKINA MURA KAZI KWENU BWANA, IRA MUBADIRIKE ETI!
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 4:58 AM | Permalink | Maoni 0

Tuesday, April 21, 2009
JAMANI, Ndugu zangu mnaombwa kumsaidia huyu mpendwa Anaumwa!

MLEMAVU wa ngozi Mariamu Obedi (18)mkazi wa eneo la Nkhungu mjini Dodoma ameiomba Serikali pamoja na wanachi wamsaidie fedha kwaajili ya matibabu ya kansa ya jicho ili aweze kwenda hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar-es-Salaam kutibiwa.

Ombi hilo alilitoa jana wakati alipokuwa akizungumza na mmiliki wa blog hii mjini Dodoma huku akilia kutokana na maumivu makali anayoyapata yanayosababishwa na uvimbe uliopo katika jicho lake la kushoto kuuma.

Alikielezea kuanza kuugua jicho hilo alisema kuwa kilitokea kiupele kidogo katika jicho hilo na hivyo kuanza kuvimba ikiwa ni pamoja na kumsababishia maumivu makali.

Mariamu alisema kuwa baada yakuona hali hiyo ikizidi kuendelea aliamua kwenda katika hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma kwaajili yakupata matibabu.

Mlemavu huyo wa ngozi (albino) alifafanua kuwa alianza kuumwa mwaka 2007 ambapo alipoenda katika hospitali hiyo ya mkoa wa Dodoma uongozi wa hospitali hiyo ulimwandikia barua aende hospitali ya Mvumi.

Alisema kuwa baada ya kwenda katika hospitali hiyo ya Mvumi pia walishindwa kumtibia na hivyo kumuandikia barua wakimtaka aende jijini Dar-es-Salaam katika hospitali ya Msasani ambapo alikwenda na kufanyiwa oparesheni na kupata nafuu.

Alibainisha kuwa baada ya kupata naafuu alirejea tena Dodoma anapoishi ambapo alikaa kwa muda wa mwaka mmoja ambapo ni 2008 na ilipofika mwaka huu hali hiyo ilimrudia tena na hivyo kulazimika kurudi tena katika hospitali kuu ya mkoa wa Dodoma.

Mariamu anafafanua kuwa alipofika katika hospitali hiyo alipimwa na hivyo kuonekana kuwa ana ugonjwa wa kansa ambapo anatakiwa kwenda hospitali ya Ocean road kutibiwa.

Hata hivyo ameiomba Serikali na watu wenye mapenzi mema ambao wataguswa na tatizo alinilonalo, kumsaidia chakula kutokana na mama yake mzazi Cahrerine Peter kutokuwa na uwezo hali ambayo inamsababisha kulala njaa licha ya yeye kunywa dawa kali na hivyo kumfanya kukosa nguvu kutokana na kukosa chakula.

KAMA UMEGUSWA KUMSAIDIA BINTI HUYU, TAFADHALI WASILIANA KUPITIA NAMBA HII' +255713358273, AU tumia akaunti hii 029201039794, NBC Bank Mazengo Branch.

Mungu akubariki sana.

 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 4:01 AM | Permalink | Maoni 1

Tuesday, December 02, 2008
Jamani ee wauza nyama Dodoma wametugomea tena wenzenu , tukitaka nyama mpaka twende Dar es Salaam!
JAMANI mlioko ughaibuni huku wenzenu karibu na waume zetu wanagoma ndani ya nyumba sijui itakuwaje, baada ya migogomo kufanyika katika maeneo mbalimbali hapa nchini zikiwemo sekta nyeti kabisa, hatimaye wafayabiashara wa Ng'ombe na uchinjaji wamegoma kuchinja ng'ombe kwa muda usiojulikana, kwa maana hiyo Dodoma hatuli nyama tena hadi watakapoamua sijui itakuwa lini hiyo, hebu Jimuvuzishe hapa kwa habari zaidi!

Na Martha Mtangoo, Dodoma

12/2/2008

UMOJA wa wafanyabiashara wa uchinjaji Ng’ombe Dodoma, (UWANDO), wamesitisha huduma ya kuchinja Ng’ombe na kuuza nyama kutokana na kupandishwa ushuru katika machinjio ya kisasa na hivyo kuufanya mji wa Dodoma kukosa nyama kwa muda usiojulikana.

Wafanyabiashara hao wamepandishiwa ushuru kutoka sh 10,000 waliyokuwa wakilipa awali hadi kufikia sh 20,000 kwa ng’ombe mmoja kuanzia juzi.

Wakiongea na waandishi wa habari jana katika eneo la mnada wa mifugo wafanyabiashara hao walisema kuwa walikuta tangazo juzi katika machinjio ya kisasa kuwa kuanzia juzi wanatakiwa kulipia huduma ya uchinjai y ash 20000 kwa kila Ng’ombe.

Mwenyekiti wa UWANDO Taita Ikoyi, alisema kuwa baada ya kuona tangazo hilo walishtushwa na kuamua kusitisha uchinjaji wa Ng’ombe kutokana na gharama za uchinjai kuwa kubwa ikilinganishwa na bei ya mifugo ilivyo sasa.

“Sisi hatujagoma ila tumeamua kusitisha huduma ya kuchinja mifugo yetu na kupeleka nyama katika mabucha kutokana na bei ya ushuru kuwa kubwa, tunabebeshwa mzigo mkubwa sana tunaiomba serikali itufikirie na sisi wadau itupunguzie ushuru” alisema Taita.

Naye Katibu wa UWANDO, Charles Laizer alisema kuwa tangu kujengwa kwa machinjio hiyo ya kisasa wamekuwa wakilazimishwa kupeleka mifugo yao kwenda kuchinjwa katika machinjio hiyo jambo ambalo limekuwa likiwakandamiza mno.

Laizer alisema kuwa awali baada ya kuanzishwa kwa machinjio hiyo walielezwa kuwa kuna uchinjai wa aina tatu ambapo moja ya uchinjai huo ulikuwepo ule wa kawaida kwa wafanyabiashara ambapo walitegemea uchinjaji huo ungekuwa wa bei y ash 1500 kama ilivyokuwa hapo awali lakini imekuwa tofauti na matarajio yao.

“Kama hali yenyewe ndio hii ni bora manispaa ijenge machinjio nyingine yenye ushuru wa bei nafuu na sisi wadu pia tuko tayari kujenga machinjio yetu ilimradi serikali itueleze utaratibu ukoje”alisema.

Naye Kaimu Meneja wa machinjio hiyo Florian Tillya alikiri kupandishwa kwa ushuru katika machinjio yake na kudai kuwa hali hiyo imetokana na mwekezaji ambaye anamiliki macnjio hiyo kampuni ya ya uwekezajiNICO kwa pamoja na Ranchi ya taifa ya NARCO.

Tillya alisema kuwa wafanyabiashara hao walipewa taarifa ya kupandishiwa bei ya ushuru tangu tarehe 8 Novemba mwaka huu machinjio hiyo ilipobinafsishwa na kuwa ushuru huo ulitakiwa kulipwa tangu kuanzishwa kwa machinjio hiyo mwaka 2003 lakini serikali ilikataa na ilikuwa ikitoa ruzuku y ash 9000 na fedha zilizoba walikuwa wakilipia wafanyabiashara hao.

Alisema kuwa kupanda kwa ushuru huo kunasababishwa na gharama za uendeshaji wa machinio kupanda ambapo alisema kuwa bei ya mafuta, na mishahara ya wafanyakazi viko juu kwa hiyo mwekezaji ameamua kupandisha ushuru kuanzia Desemba moja.

Ends………
 
Muandishi: Martha Mtangoo |Saa:- 3:20 AM | Permalink | Maoni 4



Jina: Martha Mtangoo
Kutoka: Dodoma, Tanzania

Habari zangu zaidi..
KUMBU KUMBU
MAGAZETI TANDO

VYOMBO VYA HABARI

TAFUTA


MASIKANI


Jina:

URL au E - mail:

Ujumbe:

BLOG IMETENGENEZWA NA:


MWISHO